
Wakili wa Kujitegeme, Iddi Msawanga(kulia) akimuapisha Japhet Kembo (aliyenyanyua mkono) kuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Migombani, katika hafla iliyofanyika nje ya ofisi za mwenyekiti wa mtaa huo, Segerea Mwisho Dar es Salaam . Japhet aligombea nafasi hiyo kupitia chama cha Chadema
Siku moja baada ya wakazi wa Mtaa wa Segerea-Migombani jijini hapa kumwapisha mwenyekiti wao kwa kumtumia wakili wa kujitegemea, mapya yameibuka.
Uapishaji huo uliofanyika juzi nje ya ofisi za
serikali ya mtaa huo, mbele ya umati wa watu na waandishi wa habari,
umepingwa na ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Ilala iliyosema
kuwa ni batili.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la
Segerea, Gango Kidera alisema jana kuwa wakazi wa mtaa huo wataendelea
kupata huduma za kiserikali kutoka ofisi hiyo kama kawaida, kwa kuwa
kitendo hicho kilizingatia sheria za nchi.
“Tunasubiri tuone mkurugenzi anataka kumweka nani
badala ya kiongozi ambaye wananchi wamemchagua. Sababu za kutowaapisha
viongozi waliochaguliwa hazijitoshelezi ndiyo maana wananchi
wameshinikiza aapishwe na wakili wa kujitegemea na sheria zinaruhusu kwa
kuwa zinataka mtu anayefanya hivyo ama awe hakimu au kamishna wa
viapo,” alisema Kidera na kuongeza:
“Endapo kutakuwa na utata wowote utakaojitokeza
baada ya mwenyekiti na wajumbe wake kuanza kutekeleza majukumu yao, basi
nguvu ya umma itatumika kuamua hatma ya hali hiyo, tutaandamana na
wananchi wanasubiri kuona hilo linatokea.”
Akizungumzia sababu zilizowasukuma kutafuta wakili badala ya kusubiri uchunguzi wa halmashauri, Kidera alisema kumbukumbu za ‘uchakachuaji’ wa matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita bado hazijafutika.
Alipotafutwa Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk
Makongoro Mahanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kazi na ajira ili aeleze
kama anautambua uongozi uliosimikwa mtaani kwake, alidai kuwa
kilichofanywa ni uvunjaji wa sheria za nchi, jambo ambalo haliwezi
kuvumiliwa. Alisema mkurugenzi ndiye mwenye mamlaka ya kutangaza na
kusimamia uchaguzi ikijumuisha pia kuapisha washindi kupitia wakili
atakayemchagua na siyo vinginevyo, amewasihi Chadema kama waliweza
kufuata utaratibu tangu mwanzo, ni vyema wakavuta subira kwa kumpa
nafasi mkurugenzi ajiridhishe na uchunguzi wake anaoendelea kuufanya.
“Siwezi kupanga kubadili matokeo. Wanaosema hivyo wana uoga,” alisema Dk
Mahanga.
Ni woga tu ndiyo unaowasumbua kwasababu jina langu ni kubwa sana huku Segerea ndiyo maana wanaweweseka,” alisema Dk Mahanga.
Waziri huyo alisema kuwa haiwezekani kiongozi
aapishwe barabarani na kama hilo linapata kibali mbele ya uongozi wa juu
wa chama husika basi inewezekana tu kama wangefanya hivyo hata kabla ya
uchaguzi kufanyika ili waeleweke kuwa ni wapindisha sheria, vinginevyo,
wafuate utaratibu.
0 comments:
Post a Comment