Pages

Subscribe:

Wednesday 21 January 2015

KITUO CHA POLISI IKWIRIRI CHAVAMIWA NA MAJAMBAZI, ASKARI WAWILI WAUWAWA



Mfano wa bunduki aina ya SMG zilizoibiwa.



Mfano wa bunduki aina ya SAR zilizoibiwa na majambazi.
Mfano wa bunduki aina ya Shotgun iliyoibiwa na majambazi.
MAJAMBAZI yaliyojihamu kwa silaha yamevamia Kituo cha Polisi cha Ikwiriri, Rufiji mkoani Pwani na kuua askari wawili na kupora silaha zilizokuwepo kituoni hapo.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo, huku askari wanaodaiwa kupotenza maisha ni Cop. Edgar aliyekatwa mapanga na WP Judith aliyepigwa risasi ubavuni upande wa kulia na kutokea upande wa kushoto.
Hivi sasa hali ni tete katika eneo hilo na watu wamekusanyika huku polisi wakiongeza nguvu kusaka wauaji katika tukio la uvamizi, kituo cha polisi Ikwiriri, Rufiji, Pwani.
Silaha zilizoporwa ni SMG 2, SAR 2, SHORTGUN 1, silaha 2 za mabomu ya machozi na risasi 60 za SMG.

0 comments:

Post a Comment