
Hivi karibuni nilialikwa kwenye makulaji ya kumaliza mwaka yaliyoandaliwa jijini hapa na Wafanyakazi wa Nice Catering Company yanye Makao Makuu yake Dar es Salaam.
Ilikuwa mara ya kwanza kuisikia kampuni hiyo, lakini nilipigwa na butwaa baada ya kupata taarifa kwamba ni kampuni kubwa ambayo ina wafanyakazi zaidi ya 700 wa kudumu katika maeneo mbalimbali nchini.
Risala ya wafanyakazi ilisema kampuni yao ina
miaka 15 tangu kuanzishwa kwake na inatoa huduma za vyakula katika
vikosi kadhaa vya jeshi, inamiliki hoteli, mabasi ya kusafirisha abiria
na malori ya kubeba mafuta, vituo vya kuuza mafuta, maduka ya nguo
katika majiji ya Arusha na Dar es Salaam.
Kwa kifupi ilielezwa kwamba ni kampuni
inayoendeshwa na vijana wasomi wa kuanzia stashahada hadi shahada mbili
na ina mameneja karibu 20.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo,
Yona Sonelo akizungumza kwenye hafla hiyo alitoboa siri yake moja ambayo
kwa kweli iliwaacha midomo wazi watu wengi.
Ni kweli mshangao uliwakumba waalikwa mbalimbali
akiwamo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya ambaye alifika hapo kwa niaba ya mkuu wa
mkoa aliyealikwa aje atoe zawadi kwa wafanyakazi bora wa kampuni hiyo.
Kauli ya Sonelo iliyowashtua wengi ilisema,
“Kampuni yangu inaendeshwa na vijana wasomi wa kuanzia stashahada,
shahada moja hadi mbili, lakini mimi nimemaliza vidato vitano tu,”
alisema.
Sonelo anasema alianzisha kampuni Machi, 2000 kwa
shida kubwa, lakini alizingatia kwamba polepole ndiyo mwendo. Anasema
aliweka mkakati wa kuajiri vijana wenye ubunifu wa biashara ambao
walioondoa ujinga wa kufikiria ajira baada ya kumaliza vyuo vikuu.
“Kwa hivyo moja ya sifa za walioajiriwa
niliwauliza, baada ya kusoma walitarajia kufanya nini, waliotoa mipango
ya kazi ndiyo niliowaajiri, lakini waliosema wanatafuta kazi
zikuwataka,” anasema.
Anasema hadi sasa ana msimamo huo kwa sababu
anatambua wazi kwamba kusoma kwenye vyuo vikuu ni fursa ya kuondoa
kabisa ujinga na siyo fursa ya kuanza kutafuta kazi.
“Kwanza nina uhakika vijana wanaomaliza vyuo kila
mwaka ni wengi mno, wanafikia hata 100,000. Je, ni kweli wote wanaweza
kupata kazi Serikalini,’’ alihoji.
Anasema hata ije Serikali ya aina gani, kamwe
haiwezi kutatua tatizo la ajira kwa vijana wote wanaomaliza vyuo vikuu
bali kinachotakiwa ni kwa wahitimu wenyewe kukaa chini na kubuni kazi za
kufanya.
“Jamani tusishangae vijana kukosa ajira Tanzania, hata nchi
jirani ya Kenya wapo vijana wenye shahada wanaouza mitumba na huko
Nigeria wapo wenye shahada wanaofanya kazi ya kufagia barabarani.
“Lakini pia wapo vijana waliobuni miradi na hatimaye kusaidiwa na Serikali katika kufanikisha malengo,” anasema.
Sonelo anaishauri Serikali kwamba pamoja na
mazingira mazuri ya uwekezaji, itoe kipaumbele ya kuwasaidia kwa fedha
wahitimu nchini waweze kuwekeza kwenye miradi waliyoibuni ili watoe
ajira kwa vijana wenzao.
Hoja hiyo inafafanuliwa pia na Mkuu wa Wilaya ya
Mbeya, Dk Norman Sigalla anasema ni kweli Serikali ina wajibu wa
kuhakikisha mazingira mazuri ya uwekezaji yanatolewa kwa Watanzania.
Dk Sigalla akitoa angalizo anasema, asilimia 60 ya matajiri duniani ni wale ambao hawakufika hata chuo kikuu.
Anasema wafanyabiashara wengi waliofanikiwa ni
wale wasio na shahada na shahada za uzamili au uzamivu na kwamba wengi
ni watu wa kawaida.
“Maendeleo ya mtu yanatokana na mtu mwenyewe kujua
kutafisiri kwa usahihi matatizo ya jamii na hatimaye kutafuta
ufumbuzi,” anasema na kuongeza kwamba tatizo la wahitimu wengi wa vyuo
vikuu wa sasa bado wana imani za kizamani kutaka kuwatumikia watu
wengine.
“Enzi za Mwalimu, wasomi walikuwa wachache na
ndiyo maana hata mtumishi akifanya madudu hapa alipata uhamisho kwenda kwingine, lakini sasa hivi nafasi zimejaa kila mahali, hivyo wahitimu wa vyuo vikuu wawe na mtazamo wa kijiajiri na kuajiri wengine,” anasema.
ndiyo maana hata mtumishi akifanya madudu hapa alipata uhamisho kwenda kwingine, lakini sasa hivi nafasi zimejaa kila mahali, hivyo wahitimu wa vyuo vikuu wawe na mtazamo wa kijiajiri na kuajiri wengine,” anasema.
0 comments:
Post a Comment